• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mapato ya Ndani Kujenga Miradi ya Kimkakati

Posted on: March 4th, 2021

Mapato Ya Ndani Kujenga Miradi Ya Kimkakati

Halmashauri ya Mji wa Geita katika kipindi cha pili ndani ya Serikali ya awamu ya tano imejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati kwa kutumia chanzo cha mapato ya ndani ya Halmashauri tofauti na hali iliyokuwepo awali.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mheshimiwa Costantine Morandi wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani robo ya pili kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Ofisi kuu Halmashauri ya Mji Geita.

Mhe. Morandi amesema kuwa miradi mikubwa kama ujenzi wa masoko na machinjio ya kisasa imetekelezwa kupitia fedha zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita kwa jamii inayowazunguka( CSR) lakini Halmashauri ya Mji inaongoza katika ukusanyaji wa mapato kuliko Halmashauri zote za Miji Tanzania Bara, hivyo inatakiwa fedha hizo zifanye mambo makubwa na ya mfano.

“Halmashauri ya Mji Geita tumepanga kutoka kwenye dhana ya CSR na kufanya thamani ya makusanyo yetu ya ndani kuonekana, tunatakiwa tujenge Zahanati nzuri na za kisasa, Shule za msingi na Sekondari, masoko ya kisasa pamoja na miradi mingine kuanzia msingi mpaka ukamilishaji kwa kutumia fedha za mapato ya ndani tukisaidiwa na nguvu za wananchi na si kutegemea fedha za CSR katika kutekeleza miradi hiyo”. Aliongeza Mhe. Morandi.

Akisoma changamoto mbalimbali zilizopo katika kata zote za Halmashauri ya Mji wa Geita, Diwani wa Kata ya Nyanguku Mheshimiwa Elias Ngole amesema kuwa upungufu wa vyumba vya madarasa kwa shule zote na ubovu wa mabarabara ambazo zimeharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha ni miiongoni mwa vikwazo vinavyowakabili wananchi walioko kwenye maeneo yao ya utawala.

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Magreth Macha amesema kuwa Halmashauri ya Mji Geita itaendelea kukabiliana na changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa kwa kujenga vyumba zaidi kulingana na upatikanaji wa fedha. Kadhalika Mamlaka ya Elimu Tanzania  imeridhia kujenga Mabara moja ya masomo ya sayansi katika Shule ya Sekondari Nyanza.

Katika hatua nyingine Halmashauri ya Mji wa Geita imetenge shilingi 150,000,000/= katika bajeti yake ya mwaka 2021/2022 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Shiloleli na shilingi 50,000,000/= kwa lengo la kununua maeneo ya kujenga shule mpya ya sekondari ndani ya Kata ya Buhalahala,




Matangazo

  • Fomu za Kuijiunga Kidato cha Kwanza Shule ya Sekndari Nyankumbu na Geita December 29, 2020
  • TANGAZO LA KODI YA MAJENGO April 20, 2018
  • TANGAZO LA WAMILIKI WA VIWANJA VILIVYOSHINDWA KUENDELEZWA BOMBAMBILI NA MAGOGO May 28, 2018
  • TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI YA HESABU ZA KUISHIA TAREHE 30 JUNI 2017 June 29, 2018
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Taasisi Za Fedha Kopesheni Kwa Riba Nafuu- DC

    March 12, 2021
  • Mapato ya Ndani Kujenga Miradi ya Kimkakati

    March 04, 2021
  • Wananchi Wakumbushwa Kulipa Kodi Kwa Muda

    March 02, 2021
  • Geita Mji Yajipanga Kuepuka Mrundikano wa Wanafunzi

    February 15, 2021
  • Zaidi

Video

Bombambili Bomba ndani ya Miaka 5 ya JPM
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa