• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Watendaji Watakiwa Kusimamia Vyema Mkataba Wa Lishe

Posted on: October 28th, 2022

Watendaji Watakiwa Kusimamia Vyema Mkataba Wa Lishe

Watendaji wa Kata 13 za Halmashauri ya Mji wa Geita wameagizwa kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa viashiria vyote vilivyomo katika mkataba wa lishe ili kuleta mabadiliko katika kuboresha hali ya lishe kuanzia ngazi ya kaya hadi jamii nzima pamoja na kuweka utaratibu maalum wa kuadhimisha siku ya lishe kwa kila kata.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Zahara Michuzi hivi karibuni alipokuwa akishuhudia tukio la watendaji wote wa kata kusaini mkataba wa lishe, tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano katika jengo la ofisi ya Halmashauri ya Mji Geita eneo la Magogo Geita mjini.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita ameeleza kuwa viashiria vinavyotakiwa kutekelezwa ni pamoja na Watoto kupatiwa chakula mashuleni, wakina mama wajawazito kuhudhuria kliniki ipasavyo na kupatiwa madini joto, Watoto kupatiwa vitamin A, Watoto wenye utapiamlo mkali kupatiwa huduma vituoni na utoaji wa fedha ipasavyo kwa ajili ya afua za lishe.

“Watendaji wote hakikisheni mnasimamia vigezo vya upimaji na vipaumbele vya kata kwa kila mwaka ambavyo ni upatikanaji wa taarifa za hali ya lishe kwa Watoto chini ya miaka mitano, kufanya ufuatiliaji wa Watoto walioacha matibabu ya utapiamlo kwa kushirikiana na watoa huduma za afya ngazi ya jamii.” Aliongeza Bi. Zahara Michuzi.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Geita Oscar Obeid amesema kuwa ataendelea kujipanga Zaidi ili kuhakikisha kata zote ndani ya Halmashauri kila kiashiria kinafika asilimia 95 na sio chini ya hapo. Kadhalika kitengo chake kitaendelea kutoa elimu kwa jamii ili wazazi watambue umuhimu wa kuchangia chakula cha Watoto mashuleni ili kukuza kiwango chao cha lishe, kuongeza usikivu na kupunguza tatizo la utoro kwa wanafunzi.

Utekelezaji wa mkataba wa lishe uliosainiwa utakuwa wa miaka nane kuanzia tarehe mosi Julai 2022 hadi tarehe 30 Juni 2030 kulingana na malengo na shabaha zilizoainishwa katika mikakati ya kitaifa ya muda mfupi, muda wa kati pamoja na muda mrefu ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo yam waka 2025, mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala na Sera mbalimbali za nchi.



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 February 06, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Kamati Ya Siasa Mkoa Yakoshwa na Miradi Geita Mjini

    February 06, 2023
  • Wananchi Waaswa Kujitoa Katika Ujenzi Wa Miradi

    January 27, 2023
  • Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

    January 26, 2023
  • Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

    January 18, 2023
  • Zaidi

Video

Machinjio ya Kisasa Mpomvu Yaanza kazi
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa